Makala

Kuvimba miguu kwa wajawazito

0
Kuvimba miguu kwa wajawazito
Kuvimba kwa miguu

Kuvimba miguu kwa Wajawazito, hii hali huwapata zaidi ya nusu ya Wajawazito hasa miezi ya mwisho au baada ya miezi mitano

Kwanini Miguu inavimba?

Kuvimba kwa miguu hutokana na vitu vingi baadhi ya vitu hivyo ni;-

1) Wakati wa ujauzito mwili wa mama mjamzito huwa na kiasi kingi cha fluid kuliko kawaida.

2) Kuongezeka kwa pressure katika vein za miguu hasa (vena kava) vein ambayo hutoa damu kutoka kwenye miguu kupeleka kwenye moyo.

3) Kula vyakula vyenye chumvi nyingi au chumvi mbichi hasa wala chips hula sana chumvi mbichi.

4) Kusimama kwa muda mrefu

5) Kuchoka sana au kufanya kazi kwa muda mrefu.

6) Mazingira ya joto kali pia hufanya miguu ivimbe

Soma pia:  Sheria Mpya Iliyopitishwa baada ya Wanafunzi wengi Kupatwa na Ujauzito

7) Uvutaji wa sigara

8) Kutokula vyakula vyenye potassium kwa wingi kama ndizi mbivu.

9) Kutokunywa maji ya kutosha wakati Mama Mjamzito anatakiwa kunywa maji kuanzia lita tatu kwa siku na kuendelea.

10) Kutokula vyakula vyenye vitamin A na K.

Pindi utakapoona miguu imeanza kuvimba ni vizuri kwenda kituo  Afya na kufanya vipimo  kama kucheki pressure, mkojo n.k.\

kuvimba kwa miguu
kuvimba kwa miguu

Comments

Comments are closed.

More in Makala